Friday, 25 March 2016

Mtanzania ADI YUSSUF mzaliwa wa ZANZIBAR yumo nchini akitokea ENGLAND kwenye mji uitwao MASFIELD ambapo kunatimu iitwayo Mansfield Town Football Club hii ndiyo timu anayo tokea huyu MTANZANIA, Ana umri wa miaka 24 kwani alizaliwa 20 February 1992 pia nafasi anayo cheza ni mshambuliaji alianza maisha yake ya soka kwenye timu ya LEICESTER CITY tayari amejiunga na timu ya taifa kuongeza nguvu huenda akalitumikia taifa kwenye mechi ya jumatatu dhidi ya CHAD pale taifa.
Kwa mujibu wa mtandao wa SKY SPORTS nilipokuwa napekenyua undani wa mchezaji huyu msimu huu kwenye mashindano ya Capital One Cup,Sky Bet League,Johnstone's paint na The FA Cup anaidadi ya magoli 5 aliyoifungia timu hiyo inayo shiriki League Two.
Tagged

0 comments